Wednesday, January 1, 2014

Utalii:ELIMU NA HAMASA KWA WATANZANIA ITAINUA UTALII WA NDANI.

Tanzania ni moja kati ya nchi ndani ya jumuia ya afrika mashariki na afrika kwa ujumla yenye kupokea watalii kutoka pande mbalimbali za dunia.
Watalii hao hufika na kutazma vivutio mbalimbali vilivyopo katika nchi ya Tanzania.
Wageni wengi huja Tanzania kwa malengo ya KUPUMZIKA,KUFURAHI,KUFANYA UTAFITI NA KUJIFUNZA.
Wageni wengi wameonekana kuvutiwa na uzuri wa nchi ya Tanzania kutokana na vivutio vyake kama MBUGA ZA WANYAMA,MILIMA,MAZIWA,MABONDE na mambo mengine kibao ambayo hayapatikani katika nchi nyingine duniani isipokuwa Tanzania.
Wageni wengi huja kuwatazma wanyama waliopo ktk mbuga zetu na hivyo kufurahi sana wanapowaona katika macho yao.
Kwa upande wawatanzania wenyewe,muhamko wa kutembelea hifadhi au vivutio vyetu umekuwa ni mdogo sana,hali inayopelekea watanzania wachache sana kufika ndani ya hifadhi.
Hali hiyo inasababishwa na muhamko mdogo wa wa watanzania juu ya kutembelea ktk hifadhi na wengi wanaamini kuwa wazungu peke yao ndio wanapaswa kufanya utalii.
Hayo yanasababishwa na mambo mengi ikiwemo KUKOSEKANA KWA ELIMU JUU YA UTALII WA NDANI na wakati mwingine hali ya uchumi nayo inachangia kwa kiasi kikubwa kusababisha uwepo mdogo watalii wa ndani.
Kuna baadhi ya watanzania ambao wanauwezo wa kufika ndani ya hifadhi lakini bado na wao hawafiki kutokana na kutopewa elimu na hamasa ya kufika na kuzitembele hifadhi.
Kuna muonekano mkubwa,kuwa wanafunzi kwa asilimia kubwa ndio wanaotembelea ndani ya mbuga za wanyama kuliko watu wazima.
Elimu ya utalii iwapo itatumika vizuri itachangia kukuza na kuinua utalii utalii wa ndani.
Kwa maoni na ushauri wasiliana nasi kwa barua pepe:ningawildlifefoundation@gmail.com au simu namba +255755519736 pia unaweza kulike page yetu ya NINGA WILDLIFE FOUNDATION ktk mtandao wa www.facebook.com

No comments:

Post a Comment